Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakiri makosa, watakiwa kulipa Sh300 milioni

81463 MAKOSA+PIC Wakiri makosa, watakiwa kulipa Sh300 milioni

Thu, 24 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu  Donald Njonjo na mfanyabiashara wa Tandika sokoni, Gamba Muyemba kulipa fidia ya Sh300 milioni baada ya kukiri kosa la kuuza madini bila kibali.

Njonjo ambaye ni meneja ukaguzi wa shughuli za maabara Wizara ya Madini na mwenzake wamehukumiwa leo Jumatano Oktoba 23, 2019 na hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo, Kelvin Mhina.

Hakimu huyo aliamuru washtakiwa hao kulipa Sh50 milioni leo, jambo ambalo walilitekeleza.

Kiasi kilichobaki cha Sh250 milioni, washtakiwa hao  wanatakiwa kukilipa kwa awamu ndani ya miezi 12 kuanzia leo.

Pia, mahakama hiyo imetaifisha mali za mshtakiwa Donald ambazo ni viwanja viwili  ploti namba 51/1/bloc C kilichopo  Njedengwa high Density Dodoma na kingine kilichopo eneo la Nzuguni B Dodoma.

Vingine vilivyotaifishwa ni gari aina ya Nissan Hard Body na kwamba vyote vitakuwa  mali ya serikali.

Pia Soma

Advertisement

Mahakama hiyo pia imetaifisha madini feki ya dhahabu feki yenye uzito wa kilogramu 2,794.5.

Hakimu Mhina amesema kila mshtakiwa anatakiwa kulipa faini ya Sh5 milioni na iwapo watashindwa watatumikia kifungo cha miaka mitatu jela.

Chanzo: mwananchi.co.tz