Zaidi lita 100 za pombe haramu ya gongo iliyotengenezwa kwa kutumia bibo zimetekezwa na wakimbiza mwenge kitaifa baada ya kesi kumalizika katika Mahakama mbalimbali mkoani Mtwara.
Zaidi lita 100 za pombe haramu ya gongo iliyotengenezwa kwa kutumia bibo zimetekezwa na wakimbiza mwenge kitaifa baada ya kesi kumalizika katika Mahakama mbalimbali mkoani Mtwara. Akitoa taarifa hiyo mbele ya Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa, Abdallah Shaib wakati wa zoezi la kuteketeza gongo hizo Koplo Lameck Mwita kutoka Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara Kitengo cha Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Madawa ya Kulevya amewataka wananchi wanaofanya biashara hiyo na wale wanaotengeneza wajue kuwa ni kinyume cha sheria.