Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakili asema Kabendera bado anajadiliana na DPP

93256 Pic+kabendera Wakili asema Kabendera bado anajadiliana na DPP

Tue, 28 Jan 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Wakili wa Serikali, Gloria Mwenda ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa majadiliano kati ya ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka (DPP) na mwandishi wa habari nchini Tanzania, Erick Kabendera bado unaendelea.

Katika kesi hiyo Kabendera anakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la utakatishaji wa zaidi ya Sh173 milioni.

Leo Jumatatu Januari 27, 2020 Kabendera aliyekuwa amevaa suruali ya bluu na tisheti ya kijivu amefikishwa mahakamani hapo huku Mwenda akisema kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutajwa kwa kuwa upelelezi haujakamilika.

Katika maelezo yake, Mwenda amesema majadiliano kati ya mshtakiwa na DPP bado yanaendelea, kuiomba mahakama kuipangia kesi hiyo tarehe nyingine.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 10, 2020.

Kwa mara ya kwanza Kabendera alifikishwa mahakamani hapo Agosti 5, 2019 akikabiliwa na makosa hayo anayodaiwa kuyafanya kati ya Januari 2015 na Julai 2019, jijini Dar es Salaam.

Habari zinazohusiana na hii

Advertisement
Katika shtaka la kwanza anadaiwa katika kipindi hicho, alijihusisha  na mtandao wa uhalifu kwa kutoa msaada kwa genge la uhalifu kwa nia ya kujipatia faida.

Shtaka la pili anadaiwa katika kipindi hicho bila ya sababu alikwepa kodi ya Sh173.2 milioni aliyotakiwa kulipa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Katika shtaka la tatu, anadaiwa kutakatisha Sh173.2 milioni huku akijua fedha hizo ni mazalia ya kosa la kujihusisha na genge la uhalifu na utakatishaji fedha.

Chanzo: mwananchi.co.tz