Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu wafanyakazi wanne wa Benki ya Akiba tawi la Ilala kulipa fidia ya Sh62 milioni baada ya kukiri kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Pia mahakama hiyo imewahukumu kulipa faini ya Sh200, 000 kila mmoja na wakishindwa watumikie kifungo cha mwaka mmoja gerezani.
Washtakiwa hao ni Frank Kihedu, Wahenda Ally, Abdilla Amanzi na Isabela Ladislaus.
Hukumu hiyo imetolewa leo Jumatatu Machi 30, 2020 na Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Rashid Chaungu.
Chaungu amesema kwa kuwa washtakiwa hao wamekubali kosa mahakama inawahukumu kulipa faini ya Sh200,000 au kutumikia kifungo cha mwaka mmoja gerezani .
Chaungu alisema pia makubaliano mliyoingia na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) yatekelezwe kwa kufidia hasara waliyosababisha na kutakiwa kulipa Sh62 milioni.
Pia Soma
- Waziri, gavana Somalia wajeruhiwa na al- Shabab
- Walioambukizwa corona Rwanda wafika 70
- Ilani ya uchaguzi yatumika kwa mara ya pili