Fri, 6 Nov 2020
Chanzo: habarileo.co.tz
POLISI mkoani Tabora inawashikilia watoto 11 wenye umri chini ya miaka 14 kwa tuhuma za kujiusisha kwenye matukio ya uvunjaji,wizi na unyang’anyi .
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Barnabas Mwakalukwa alisema kuwa watoto hao ambao wengi ni wanafunzi, walipokamatwa na kuhojiwa walikiri kuhusika na matukio hayo kwa kushirikiana na watu wengine ambao ni kaka zao.
Mwakalukwa alisema walikamatwa Novemba 3 saa 10 usiku mtaa wa Kariakoo kata Kitete baada ya kuvunja nyumba ya askari mstaafu, Hussei nKatanga na kuiba kompyuta mpakato, simu na kifaa cha umeme wa jua
Chanzo: habarileo.co.tz