Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Vigogo Chadema wamkataa hakimu

10578 Vigogo+pic TanzaniaWeb

Tue, 3 Jul 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Vigogo tisa wa Chadema akiwemo mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe wamewasilisha ombi la kutaka Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri kujitoa kusikiliza shauri lao.

Kufuatia ombi hilo, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imepanga Julai 5, 2018 kutoa uamuzi katika kesi inayowakabili viongozi hao.

Uamuzi huo wa mahakama umetolewa leo Jumatatu Julai 2, 2018 na Mashauri baada ya  washtakiwa hao  kueleza sababu ya kutokuwa na imani nae.

“Baada ya kusikiliza sababu za washtakiwa walizotoa hapa mahakamani za kumtaka hakimu anayeendesha shauri hili kujitoa, Julai 5 mahakama hii itatoa uamuzi kama hakimu huyo ajiondoe kuendesha shauri hilo au asijiondoe” amesema hakimu Mashauri.

 

Wakili wa utetezi, Peter Kibatala amesema wateja wake wamemueleza kuwa hawana imani na hakimu Mashauri anayeendesha kesi hiyo na wanaomba ujitoe kusikiliza shauri hilo, hivyo wanaomba nafasi ili waweze kueleza sababu za kutokuwa na imani nae.

 

Aliyeanza kueleza sababu za kutokuwa na imani na hakimu huyo ni Mbowe ambaye alidai kuwa ana sababu kumi.

Baada ya kupitia hoja za pande zote ambazo pia zilitolewa na washtakiwa wengine, Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi Julai 5, 2018  atakapotoa uamuzi.

Washtakiwa katika Kesi hiyo  ni Mbowe, naibu makatibu wakuu, Salum Mwalimu (Zanzibar) na John Mnyika (Bara); mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche; mbunge wa Kawe, Halima Mdee; mbunge wa Bunda, Esther Bulaya.

Wengine ni Katibu Mkuu wa Chama hicho, Dk Vicent Mashinji;  mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa na mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko.

Washtakiwa kwa pamoja  wanakabiiwa na mashtaka 13.

 

 

Chanzo: mwananchi.co.tz