Dar es Salaam. Upelelezi katika kesi ya kutekwa kwa Mfanyabiashara Mohammed Dewji 'Mo' ,bado haujakamilika.
Wakili wa Serikali Daisy Makakala amedai hayo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na ameiomba tarehe nyingine ya kutajwa.
Katika hatua nyingine wakili huyo alidai bado wanaendelea kuwatafuta washtakiwa wengine ili waunganishe katika kesi hiyo.
Awali mahakama hiyo ilitoa hati ya kuwakamata washitakiwa hao ambao ni Henrique Simbine, Daniel Manchice, Issac Tomo na Zacarious Junior wote raia wa Msumbiji na Phila Tshabalala ambaye ni raia wa Afrika Kusini.
Mmoja wa washtakiwa hao ambaye ameshafikishwa mahakamani hapo ni dereva wa taksi , mkazi wa Tegeta Mousa Twaleb.
Kesi hiyo imepangwa Oktoba 15 mwaka huu.
Pia Soma
- VIDEO: Makonda asisitiza ukaguzi vyombo vya moto, akumbuka ajali ya Morogoro
- Matano mapya katika Kongamano la gesi na mafuta Tanzania
- Watoto wa miaka minne Ghana kufundishwa elimu ya uzazi
Pia inadaiwa Oktoba 11, 2018 maeneo Hoteli ya Colloseum wilayani Kinondoni Dar es Salaam, Twaleb pamoja na watu wengine ambao hawapo mahakamani, walimteka nyara MO kwa nia ya kumuhifadhi kwa siri na kumuweka maeneo ambayo ni hatari.
Pia inadaiwa Julai 10, 2018 maeneo ya Mbezi Beach wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, Twaleb alitakatisha fedha ambazo ni Sh 8,000,000 wakati akijua fedha hizo ni kosa la kushiriki genge la uhalifu na makosa ya kupanga.
MO alitekwa nyara Oktoba 11, 2018 alfajiri maeneo ya Hoteli ya Colloseum wakati akienda kufanya mazoezi na alipatikana Oktoba 20, mwaka huo huo katika eneo la Gymkhana.
Soma zaidi: Watano kuongezwa kesi ya kutekwa Mo Dewji