Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Upelelezi kesi ya Sabaya wakamilika, mahakamani tena Julai 02

76a70a2bcbc93eb984d3736df3c1ac1f.jpeg Upelelezi kesi ya Sabaya wakamilika, mahakamani tena Julai 02

Fri, 18 Jun 2021 Chanzo: www.habarileo.co.tz

UPELELEZI wa kesi moja ya unyang'anyi wa kutumia silaha kati ya kesi tano zinazomkabili aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya, umekamilika na kwamba ameanza kusomewa maelezo ya awali ya kesi hiyo.

Hayo yamejiri leo Juni 18, 2021, Jijini Arusha wakati kesi yake pamoja na wenzake watano ilipofikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kwa ajili ya kutajwa tena kwa mara ya pili.

Sabaya na wenzake watafikishwa tena Mahakamani Julai 2, 2021.

Sabaya na wenzake watano wanakabiliwa na mashtaka matano likiwemo la uhujumu uchumi na walipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Juni 4 mwaka huu.

Chanzo: www.habarileo.co.tz