Dar es Salaam. Upande wa mashtaka katika kesi ya mauaji inayomkabili Mfanyabiashara Hamis Said (38) umedai upelelezi wa shauri hilo umekamilika na jalada la shauri hilo lipo kwenye hatua ya uchapaji.
Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon amedai hayo leo Jumatatu Oktoba 21, 2019 mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam kuwa shauri lilikuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi umekamilika.
Simon amedai jalada la shauri hilo lipo kwenye hatua ya uchapaji kwa ajili ya maandalizi ili lipelekwe Mahakama Kuu ya Tanzania hivyo ameiomba mahakama hiyo ihairishe kesi hiyo.
SOMA ZAIDI: Anayedaiwa kumuua mkewe, kumchoma moto ataka fedha zake kwenye simu
Hakimu Mkazi Mkuu, Salum Ally aliahirisha shauri hilo hadi Novemba 4, 2019.
Pia Soma
- RC Chalamila ampa saa 24 DED kuhamisha ofisi
- Jiji la Dodoma lang'ara ukusanyaji mapato, Waziri Jafo ataka wakurugenzi kujitathimini
- Kiongozi wa upinzani Sudan Kusini atishia kujitoa kwenye serikali ya mseto
SOMA ZAIDI: Anayedaiwa kumuua mkewe kisha kumchoma moto awatolea uvivu waandishi wa habari mahakamani