Dar es Salaam. Upelelezi wa kesi ya kutekwa kwa mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania, Mohamed Dewji ‘Mo’ inayomkabili dereva teksi, Mousa Twaleb haujakamilika.
Wakili wa Serikali Daiys Makakala amedai leo Jumanne Julai 11,2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kuomba tarehe nyingine.
Baada ya maelezo hayo hakimu Shaidi ameahirisha kesi hiyo hadi Juni 25, 2019 na mshtakiwa huyo kurejeshwa rumande.
Twaleb anakabiliwa na mashtaka matatu ikiwemo kumteka nyara Mo.
Mo alitekwa Oktoba 11, 2018 maeneo ya Hoteli ya Colosseum alikokwenda kufanya mazoezi na kupatikana siku tisa baadaye baada ya watekaji kumtelekeza katika viwanja vya Gymkhana.