Wed, 18 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza linawashikilia watu tisa kwa makosa mbalimbali ikiwemo wizi wa vifaa katika mradi wa Reli ya kisasa SGR.
Aidha katika hatua nyingine Jeshi la Polisi mkoani Mwanza limefanikiwa kukamata lita 4,426 za mafuta aina mbalimbali ikiwemo Diesel na Petrol.
Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Jeshi la Polisi Wilbroard Mutafungwa amesema kuwa oparesheni hiyo ilianza tarehe Jan. 11, 2023 katika maeneo ya vijiji vya Isunga Nkalalo-Bukwimba, Malya na Usagara katika Wilaya ya Kwimba na Misungwi .
Chanzo: www.tanzaniaweb.live