Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

TikTok matatani vifo vya watoto

Vifo TikTok .jpeg TikTok matatani vifo vya watoto

Sun, 24 Jul 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Familia mbili zimeamua kuishitaki Kampuni inayomiliki mtandao maarufu wa TikTok baada ya Watoto wao wa kike kufariki mwaka jana walipokuwa wakijaribu kurekodi challenge ya "Blackout"

Wazazi wa Arriani Jaileen Arroyo (9) wa Wisconsin Marekani na Lalani Walton (8) wa Texas Marekani wameungana na kituo cha sheria cha Wahathiriwa wa Mitandao ya Kijamii kuwasilisha kesi Mahakamani dhidi ya TikTok baada ya Watoto wao hao kufariki kwa kukosa hewa mwaka 2021 wakijaribu kurekodi 'chalenji" hiyo tata ambayo Watumiaji walikuwa wanajikaba hadi kuzimia.

Kesi hii inadai kuwa kampuni ya TikTok ilikuza chalenji kwa Watumiaji wake katika juhudi za kuongeza ushiriki wao na kuongeza faida ya TikTok lakini imesababisha Wasichana hao kufariki "TikTok kwa hasira haikuchukua na/au hatua isiyotosheleza kabisa kuzima na kuzuia kuenea kwa chalenji hiyo”

Maelezo yaliyopatikana kwenye nyaraka za Mahakamani yamedai pia Tiktok ilishindwa hata kuzuia mfumo wake wa kuelekeza Watoto licha ya kutabirika kwamba kutofaulu kwa waliojaribu kuifanya kungesababisha zaidi majeruhi au vifo vikiwemo vya watoto” inasomeka kesi hiyo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live