Dar es Salaam. Imeelezwa kuwa kabla ya Naomi Marijani kuuawa, hakuwa na maelewano mazuri na mumewe.
Mwanamke huyo alitoweka nyumbani kwake Mei 15, 2019 na siku 63 baadaye Jeshi la Polisi nchini Tanzania lilidai kuwa mume wake aitwaye, Khamis Luwongo alikiri kumuua na baadaye kumchoma moto kisha kufukia majivu yake.
Luwongo anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumuua mkewe wakati uchunguzi ukiendelea.
Soma zaidi: VIDEO: Eneo linalodaiwa kufukiwa mabaki ya mwili wa Naomi Marijani
Akizungumza na Mwananchi, Frank Mdong’ola, mjumbe wa serikali ya mtaa wa Kizani, ambako wanandoa hao walikuwa wakiishi alisema alipata taarifa ya wawili hao kutokuwa na uhusiano mzuri kutoka kwa Luwongo.
“Siku ambayo alikuja ofisini kutoa taarifa kwamba mkewe ametoroka na kumuacha mtoto, tulimuuliza imekuwaje hadi mke anaondoka asimuage? Akasema kwa muda mrefu hawakuwa na maelewano,” amesema Mdong’ola.
Pia Soma
Soma zaidi: Anayedaiwa kumuua mkewe, kumchoma moto ashikiliwa polisi
Kwa habari zaidi soma gazeti la Mwananchi la leo Jumapili Julai 21, 2019