Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

TAKUKURU Arusha yaokoa zaidi y ash,bilioni 4.2

002f2e07452e87fb11a7ac04e02ff1fd TAKUKURU Arusha yaokoa zaidi y ash,bilioni 4.2

Thu, 22 Oct 2020 Chanzo: habarileo.co.tz

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Arusha,

imeweza kuokoa fedha zaidi ya sh, bilioni 4.2, kutoka kampuni

mbalimbali za utalii, ikiwemo ya uwindaji ya Otterlo Business

Corporation (OBC),vyama vya ushirika, Vikoba na Saccos, katika

kipindi cha Julai hadi Septemba mwaka huu.

Aidha fedha hizo ni pamoja na kodi za serikali, fedha za watu binafsi,

mikopo umiza na fedha za wakulima na wajasiriamali.

Kwamujibu wa taraifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana Jijini

hapa na Kaimu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Arusha, James Ruge alisema

sh,bilioni 3.5 zimelipwa na kampuni ya kitalii ya OBC,sh, milioni 60

zimelipwa na kampuni ya ANICROP Services ambazo ni kodi ya serikali

zilizokwepwa kulipwa na makampuni hayo kwa nyakati tofauti kati ya

mwaka 2018/2020.

Alisema kati ya fedha hizo pia zaidi ya sh, milioni 28.9 ni kodi na

mikopo ya serikali iliyokwepwa kurejeshwa na kufanyiwa ubadhirifu na

wananchi pamoja na watendaji mbalimbali wa serikali katika nyakati

tofauti.

Aidha kutoka vyama vya Ushirika jummla ya sh, milioni 98.9 za Chama

Kikuu cha Ushirika cha Arusha Cooperation Union (ACU) zilizokuwa

zimefanyiwa ubadhirifu baada ya mali za chama hicho kuuzwa kwa watu

wasio waaminifu na zaidi ya sh, milioni 4.3 zililipwa na Bodi ya

Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB), pamoja na sh, milioni 8 ni

michango ya wanachama wa mabaraza ya wafugaji, iliyofanyiwa ubadhirifu

na viongozi wao.

“Fedha zingine tumeziokoa kutoka VIKOBA na SACCOS ambazo ni zaidi ya

sh, milioni 86.5 ambazo ni mikopo mbalimbali iliyokuwa haijarejeshwa

kw amuda mrefu kinyume na taratibu,”.

Ruge alisema fedha zingine zimetoka kwa watu binafsi na mikopo

umiza, ambazo ni zaidi ya sh, milioni 194 zilizokuwa za madai ya watu

binafsi mbalimbali na mikopo iliyokuwa imetolewa kwa riba kubwa na

Taasisi za kifedha IVOJ Micro Credit Co Ltd ya jijini Arusha na Rhobi

Credit Co Ltd ya Karatu.

Pia madai ya wakulima na wajasiriamali wameokoa zaidi ya sh, milioni

289.2 zilizokuwa zilipwe na kampuni ya Kijenge Animal Products kwa

wakulima waliouzia kiwanda hicho bidhaa za kilimo,lakini hawakulipwa

kwa muda mrefu.

“Pia zaidi ya sh, milioni 5.9 ni fedha za wakulima waliouza mazao yao

kwa kampuni ya TBL na kampuni moja ya mbegu iliyopo wilayani Monduli

bila kupewa malipo yao,”.

Chanzo: habarileo.co.tz