Tue, 6 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Songwe: Noah Ruben Mwanjali, aliyekuwa mkusanya mapato, amehukumiwa kwenda jela miaka 8 au faini ya milioni 4 kwa kukutwa na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka, ufujaji na ubadhirifu wa fedha za umma, Tsh. milioni 26.
Hukumu hiyo ya Shauri la Uhujumu Uchumi Na. 06/2021 imetolewa Agosti 30, chini ya Hakimu Mkazi, Timoth Lion, mshtakiwa amekutwa na hatia ya kutumia fedha za umma kwa matumizi binafsi.
Aidha, mtuhumiwa amepelekwa gereza la Ilembo - Mbozi baada ya kushindwa kulipa faini.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live