Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sita kortini kwa kusafirisha bangi kilo 197.49

74440 Bangi+pic

Thu, 5 Sep 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es salaam. Wafanyabiashara watano  na dereva mmoja, wamefikishwa katika Mahakama ya  Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam Tanzania wakikabiliwa na shtaka moja la usafirishaji wa bangi.

Washtakiwa hao wamefikishwa mahakamani hapo leo Alhamis Septemba 4, 2019 na kusomewa shtaka hilo na wakili wa Serikali, Tuli Helela .

Washtakiwa hao ni Shabani Salum Juma mkazi wa Gongo la Mboto, Yahaya Majaba mkazi wa Ukonga Madafu na Ezekiel Patrick maarufu  Dudu mkazi wa Gongo la Mboto  Ulongoni A.

Wengine ni Abdul Rabi Abdulrahahim maarufu Nkupe na mkazi wa Gongo la  Mboto  Ulongoni B na Ginziari Aidan mkazi wa Kiwalani Migombani na Mnyamani Juma (30) mkazi wa Tabata Relini Dar es Salaam.

Akiwasomea shtaka hilo mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Vicky Mwaikambo, Wakili Helela amedai kuwa washtakiwa wote kwa pamoja wanakabiliwa na kesi ya usafirishaji wa  dawa za kulevya aina ya bangi.

Wanadaiwa  kutenda kosa hilo Oktoba 16, 2016 eneo la njia panda ya Segerea  wilayani Ilala.

Pia Soma

Advertisement
Helela amedai siku ya tukio washtakiwa walikutwa wakisafirisha bangi kilo 197.49 kinyume na sheria.

Hawakutakiwa  kujibu  chochote kutokana na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutokuwa na uwezo wa kusikiliza kesi hiyo.

Hakimu Mwaikambo aliiahirisha kesi  hiyo hadi Septemba 19, 2019 itakapotajwa tena na washtakiwa wamerudishwa rumande .

Chanzo: mwananchi.co.tz