Wed, 29 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jeshi la polisi mkoani Shinyanga limekamata silaha aina ya Pistol Browning ikiwa na risasi 12 ambayo ilitelekezwa na mmiliki wa silaha hiyo katika moja ya shule iliopo ndani ya manispaa ya Shinyanga.
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kamanda wa jeshi la polisi mkoani humo ACP Janeth Magomi amesema katika misako iliofanywa kwa kipindi cha mwezi mmoja walifanikiwa kukamata vielelezo mbalimbali ikiwemo gramu 2025 pamoja na kete 61 za dawa za kulevya aina ya bangi, pikipiki 11 huku kesi 19 zilifikishwa mahakamani na kupatiwa ufumbuzi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live