Dar es salaam. Jalada la kesi inayomkabili mfanyabiashara Abdul Nsembo maarufu Abdukandida na mkewe, Shamim Mwasha limewasilishwa katika ofisi ya Taifa ya mashtaka.
Shamimu ambaye ni mmiliki wa Blog 8020 Fashion na mumewe wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 36/2019.
Washitakiwa hao ambao ni wakazi wa Mbezi Beach, Dar es Salaam walifikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Mei 13, 2019.
Wakili wa Serikali mwandamizi, Wankyo Simon amedai hayo leo Ijumaa Machi 28, 2020 mbele ya Hakimu Mkazi, Vicky Mwaikambo wakati kesi hiyo ilipotajwa.
"Upelelezi wa shauri hili haujakamilika jalada limewasilishwa katika ofisi ya Taifa ya mashtaka kwa ajili kusomwa na kutolewa uamuzi wa kisheria, hivyo tunaomba tarehe nyingine ya kutajwa,” amedai wakili Wankyo
Hakimu Mwaikambo ameahirisha kesi hiyo hadi Machi 13, 2020 kwa ajili ya kutajwa.
Pia Soma
- Mwandishi ‘Mimi na Rais’ atunukiwa Tuzo ya Mabati Cornell
- Wataka mchakato wagombea viti maalum utazamwe upya
- Diamond atua studio za Swizz Beatz Marekani
Ilidai kuwa Mei Mosi mwaka 2019 maeneo ya Mbezi Beach walisafirisha dawa za kulevya zenye uzito huo huku wakijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.