Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na wenzake watatu wanaotuhumiwa kwa makosa ya ugaidi inatarajiwa kuendelea kuunguruma Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi leo Alhamisi Novemba 4, 2021.
Mahakama hiyo leo inatarajiwa kuendelea kupokea ushahidi wa upande wa mashtaka kutoka kwa shahidi wa sita.
Kesi hiyo ilishindwa kuendelea jana baada ya shahidi aliyekuwa ameandaliwa kushindwa kufika mahakamani kutokana na kuugua.
Tayari washtakiwa wameshafikishwa kwenye chumba cha mahakama na Mawakili wa pande zote pia wameshafika mahakamani mpaka sasa ni Jaji Joachim Tiganga ndiye anayesubiriwa.