Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Shahidi kesi ya kina Sabaya adai kuelekezwa kusema uongo na wakili wake mahakamani

Sabaya Piuc Data Mwahomange pia ni mshtakiwa wa tatu katika kesi hiyo

Wed, 16 Mar 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Shahidi wa saba upande wa utetezi katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya,Watson Mwahomange (27) amedai mahakamani kuwa wakili wake alimfundisha kusema uongo mahakama kwa kukana taarifa zake wakati akisomewa maelezo ya awali.

Mwahomange ametoa madai hayo jana Jumanne Machi 15, 2022 mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Patricia Kisinda wakati akiulizwa maswali na wakili wa utetezi Mosses Mahuna.

Mwahomange ambaye pia ni mshtakiwa wa tatu katika kesi hiyo, amekuwa akijitetea mwenyewe baada ya wakili wake kujitoa.

Amesema kuwa wakili wake alimueleza endapo atakubali atapewa adhabu ya kifungo cha miaka 20 jela na kwamba, Juni 19, 2021 waliposomewa maelezo ya awali, alikataa maelezo yote aliyosomewa na Wakili wa Serikali Mwandamizi Felix Kwetukia na kukubali maelezo ya kukamatwa na kufikishwa mahakamani tu.

Amedai kuwa alikataa kila alichoulizwa ikiwemo majina yake, umri wake, kabila lake na mashtaka yanayomkabili ila anachokisema kwa sasa chini ya kiapo ndiyo ukweli ikiwemo kukiri majina yake umri na kabila lake.

"Wakili wangu Fridolin Bwemelo aliniambia nikatae kila kitu kwani nikikubali nitafungwa ila kwa sasa niko chini ya kiapo ndiyo kinanizuia nisiseme uongo," amesema shahidi huyo.

ADVERTISEMENT

Sehemu ya mahojiano hayo ilikuwa kama ifuatavyo;

Wakili: Shahidi unaweza kuikumbusha mahakama majina yako

Shahidi: Watson Stanley Mwahomange na Henrick ni jina langu la ubatizo

Wakili:Ni sahihi licha ya majina hayo nyumbani kwenu unapoishi wanakuita Watii?

Shahidi: Ni sahihi maana ni kifupi cha Watson

Wakili: Sasa Bwana Watii kwanini uliacha shule form two??

Shahidi: Sikuishia Form two niliishia darasa la saba

Wakili: Shule gani?

Shahidi: Trust St.Patrick

Wakili: Kwa nini uliishia darasa la saba?

Shahidi: Nilipata matatizo (ajali) nikaacha shule

Wakili: Kwa nini hukwenda shule?

Shahidi: Nilikuwa na talent ya kupiga picha nilijifunza kupitia nilìokuwa nakaa nao

Wakili:Ulijifunza wapi uongo?

Shahidi:Uongo sijawahi kufundishwa popote

Wakili: Ni kipaji?

Shahidi: Sijui

Wakili: Ni kweli 4/6/2021 uliletwa mahakamani na kushitakiwa kwa makosa mawili? Kuunda genge na kutakatisha fedha

Shahidi: Ni kweli

Wakili: Wakati unasomewa makosa hayo 4/6/2021 wewe ulikuwa unamfahamu Sabaya?

Shahidi: Ndiyo

Wakili: Sylvester?

Shahidi:Ndiyo

Wakili: Enock?

Shahidi:Ndiyo

Wakili:Ni kweli kwamba 16/9/2021 hapa mahakamani ulisomewa maelezo ya awali hapa mahakamani?

Shahidi:Ndiyo

Wakili: Ni kweli kwamba kati ya maelezo yote yaliyosomwa na Wakili wa Jamhuri Felix Kwetukia wewe ulikataa maelezo yote ukakubali kukamatwa na kufikishwa mahakamani?

Shahidi: Ndiyo nilikataa pamoja na jina

Wakili:Ulikataa yote

Shahidi: Hayo yalikuwa maelekezo ya wakili wangu aliniambia nikatae kila kitu

Wakili:Ni kweli kwamba ulikataa jina lako, umri wako, ulikataa kabila, ulikataa makazi yako katika hayo maelezo yaliyosomwa na wakili wa Jamhuri?

Shahidi:Ni kweli nilikataa

Wakili: Jana na leo umeieleza hii Mahakama unaitwa Watson Stanley Mwahomange lakini ni sahihi jina hilo ulilikataa

Shahidi: Nililikataa kwa maelekezo ya wakili

Wakili: Wakili wako alikuwa nani?

Shahidi: Wakili ninayemjua alikuwa Fridolin

Wakili: Ulikataa umri wa miaka 27 jana ukaeleza mahakama wewe una umri wa miaka 27

Shahidi: Ni kweli

Wakili: Lakini ni kweli tarehe 16/9/2021 ulikataa?

Shahidi: Sikuwa chini ya kiapo.Nilikataa kwa maelekezo ya wakili wangu aliniambia nitafungwa

Wakili:Ni kweli kwamba ulisomewa facts zinazosema wewe unafahamiana na wenzako sita unaoshtakiwa nao ukakataa

Shahidi: Niliambiwa na Wakili niseme hivyo

Wakili: Je ni kweli ulisema hivyo?

Shahidi: Sikumbuki ila wakili aliniambia utakachokubali utafungwa usije kukubali

Wakili: Ikawaje jana ukasema unawafahamu Sabaya, Enock na Sylvester

Shahidi: Ningekuwa siwafahamu nisingekamatwa nao na jana nilikuwa chini ya kiapo

Wakili: Kwa hiyo wewe Wakili akikuambia sema uongo utasema uongo?

Shahidi: Akiniambia niseme uongo nitasema ukweli ndiyo maana aliniambia niseme uongo nikakataa

Wakili: Ulichokisema 16/9/2021 ni uongo au ukweli ambacho unasema Wakili wako alikuambia useme?

Shahidi: Ulikuwa uongo

Wakili: Ule ulikuwa uongo

Shahidi: Ndiyo. Na huu ndiyo ukweli sasa

Wakili: Wakili ndiyo alikwambia useme uongo??

Shahidi:Ndiyo aliniambia kataa aliniambia ukikubali utafungwa

Wakili:Ni uongo gani umesema hapa mahakamani

Shahidi:Sijasema uongo wewe ndo unataka niseme uongo

Wakili:Nini kinakuzuia usiseme uongo leo?

Shahidi:Niko chini ya kiapo ndiyo kinanizuia nisiseme uongo

Wakili:Ni kweli wakati wa maelezo ya awali ulikataa kukutana na Mrosso

Shahidi:Kwa kifupi nilikataa vyote kwa maelekezo ya wakili

Wakili:Sasa bwana Watson 22/1/2021 wakati wewe unasema ulipelekwa pale kwa Mrosso na hilo kundi la watu la mshitakiwa wa kwanza ni kweli PW 13 hakuwa kati ya hao watu?

Shahidi:Sikuangalia watu hivyo siwezi kujua

Wakili:Ni kweli kwamba wakati wa ushahidi wake hapa mahakamani Ramadhan alisema hakuwepo kwa Mrosso na alipata kwa kupitia taarifa

Shahidi:Ndiyo

Wakili:Ni kweli siku hiyo umeeleza mahakama jana siku hiyo ulikuwa umefungwa pingu?

Shahidi:Nilifungwa pingu na kutolewa lock

Wakili:Ulifunguliwa pingu wakati gani?

Shahidi: Nilifunguliwa pingu ndani ya gari nikabebeshwa boksi lenye pump na kupeleka ofisini kwa Mrosso

Wakili: Ulifunguliwa pingu kwenye gari la nani

Shahidi: Gari la Sabaya VX

Wakili: Kama ulifunguliwa pingu ndani ya gari utakubaliana na mimi mtu aliyepo nje ya gari hawezi kukuona ukiwa na pingu?

Shahidi: Ni sahihi

Wakili: Pw 13 Ramadhan alieleza mahakama kwamba wewe ulikuwa umefungwa pingu ukiwa kwa Mrosso.Je ulikuwa naye ndani ya gari?

Shahidi: Sikuwa naye ndani ya gari

Wakili: Wewe uliongea na Ramadhan kwa faraghà?

Shahidi: Haikuwa private kwa sababu askari alikuwepo

Wakili: Ramadhan alijuaje ulifungwa pingu?

Shahidi: Alisema kuna watu amefanya nao mahojiano ya awali na kupitia taarifa yeye ndo alipaswa aulizwe hilo swali

Wakili:Ulisikia ushahidi wa watuhumiwa wenzako wote wakisema 13 Ramadhan alienda gerezani akishawishi watuhumiwa hao waseme uongo kumkandamiza Sabaya kwa sababu wao wana nia ya kumfunga Sabaya na PW 13 aliwaambia mwenzenu mmoja ameshakubali kwamba yeye atasema uongo

Shahidi:Mimi sisemi uongo nasema ukweli.Niliwasikia wakisema hayo

Wakili:Ni kweli kwamba katika mashahidi wote wa jamhuri ambao walikuwepo kwa Mrosso kuanzia Mrosso,PW 4,PW 3 hakuna hata mmoja alisema alikuona umefungwa pingu?

Shahidi:Ni kweli

Wakili:Ni kweli wewe na Ramadhan mmepanga habari ya pingu ndiyo maana hata yeye ambaye hakuwepo eneo la tukio ndiyo anazungumzia habari ya kufungwa pingu ili umkandamize Sabaya

Shahidi:Si kweli kabisa

Wakili:Ni kweli Rama atakuambia atakutoa kwenye kesi hii na atakupa Sh10 milioni

Shahidi:Siyo kweli

Wakili: Unasema 20/1/2021 ulipeleka pump kwa Mrosso na ukasaini pale

Shahidi: Niliandika jina langu na namba za simu

Wakili:Hicho kitabu kipo?

Shahidi:Kipo

Wakili:Ni sahihi kitabu hicho kingeletwa kingethibitisha wewe kuwepo 20/1/2021?

Shahidi: Angeulizwa Mrosso.

Wakili: Unataka kutuambia PW 13 mpelelezi bwana Rama alificha hicho kielelezo hakukileta hapa mahakamani

Shahidi: Mimi siwezi kujua

Wakili: Hivi kama hicho kitabu kipo kwanini PCCB au Mrosso hawakuleta

Shahidi: Mini sihusiki na PCCB na Mrosso wangeulizwa

Wakili:Kwanini hujakiomba kwa Mrosso ulete?

Shahidi:Nitaombaje kitabu wakati siyo cha kwangu

Wakili:Simu yako iko wapi?

Shahidi:Iko Takukuru

Wakili:Hujawahi kuwa na simu

Shahidi:Umesema wewe

Wakili:Tutajie Imeu namba ya simu yako

Shahidi:Sikumbuki na sitaki kuongea uongo niko chini ya kiapo

Wakili:Una risiti?

Shahidi:Nina risiti na boksi

Wakili:Hujawahi kuwa na simu

Shahidi:Ninayo

Wakili:Una kitambulisho cha taifa wewe

Shahidi: Ninayo

Wakili: Huna

Shahidi:Heeeee

Wakili: Namba ngapi kitambulisho chako?

Shahidi: Sikumbuki

Wakili: Simu yako ilichukuliwa na nani?

Shahidi: Shabani wa PCCB

Wakil: Una uthibitisho wa Shaban kuchukua simu yako,ulipewa risiti ya nakala ya ukamataji?

Shahidi: Mimi sina

Wakili: Mahakama itajiridhishaje simu yako ilikamatwa na Takukuru?

Shahidi:Itajiridhisha kwani shahidi Shaban alisema hapa mahakamani alikamata simu yangu

Wakili: Kwa nini hukuomba hiyo hati?

Shahidi: Ndiyo mara yangu ya kwanza na sikuwahi kujua mambo ya certificate

Wakili: Shaban alisema amekamata simu 10 alisema ni ya kwako?

Shahidi:Alisema amekamata simu zao zaidi ya 10 na mimi nikiwepo

Wakili:Ni watu wangapi walikamatwa Dar es Salaam?

Shahidi: Mimi, Sylvester, Sabaya, Enock, Saitabau na mke wa Sabaya

Wakili: Ulisema ile simu ina picha ya PW 4?

Shahidi: Sikusema simu yangu ina nini ndani

Wakili: Ulivyokua unaiomba ulitaka utuonyeshe nini?

Shahidi: Ingeletwa ningeonyesha

Wakili: Jana ulisema ulimpiga picha Mzee Kazibira na kumtumia Sabaya

Shahidi:Nilipiga ili kumthibitishia Sabaya aikuwa mtaani alipokuwa anasema

Wakili: Picha iko kwenye simu yako?

Shahidi: Ndiyo iko kwenye simu yangu kwenye meseji za whatsapp

Wakili:Unataka kusema PCCB hawajui kufanya uchunguzi,wakamate simu yenye picha wasiilete mahakamani?

Shahidi:Mimi sijawahi kufanya kazi PCCB

Wakili:Baada ya kumaliza darasa la saba ulienda kozi ya kutambua sauti ya mtu kwenye electronic device?

Shahidi:Hapana

Wakili:Mtu wa darasa la saba anawezaje kujua sauti ya mtu kwenye simu?

Shahidi:Hata mtoto anajua sauti ya baba yake kwenye simu

Wakili: Ni baba yako?

Shahidi:Hapana ila sauti ya Sabaya naijua nikiwa naongea naye

Wakili: Sasa ni kweli kwamba jana ulieleza mahakama kwa muda huu hakuwahi kukupigia simu kwa simu yake?

Shahidi: Nilichoeleza ni vinavyohusiana na kesi. Amewahi kabla kunipigia ila niliyoeleza jana hakuwahi kunipigia kwa simu yake

Wakili: Unasema ulikuwa unampiga picha Sabaya alikuwa anakulipa?

Shahidi:Ndiyo

Wakili:Ulikuwa unampa risiti

Shahidi:Sina kitabu cha risiti wala Tin namba

Wakili:Umesema umewahi kumpiga picha Sabaya akiwa na Askofu Masangwa na Mchungaji Mollel

Shahidi:Ni kweli

Wakili:Ziko wapi?

Shahidi:Yeye ndo anazo nilimkabidhi Mile Stone

Wakili:Ni kweli kwamba zile picha ukipiga unaziweka kwenye laptop unatèngeneza unachukua USB unampa?

Shahidi:Ndiyo

Wakili:Ulikuwa unatumia nini?

Shahidi: Kamera Canon 7D Mark two

Wakili: Hiyo kamera na laptop ziko wapi

Shahidi: Kamera niliuza nikanunua nyingine lakini laptop ipo

Wakili: Kwanini hukuleta laptop?

Shahidi: Storage ilikua inajaa unafuta picha za mteja

Wakili: Nitakuwa sahihi nikisema ile laptop haina picha za Sabaya

Shahidi: Inazo nyingi

Wakili: Kwa nini hukuleta laptop wakati ingethibitisha ulikuwa mpiga picha wa Sabaya?

Shahidi: Kwa sababu nilitaka kuleta simu

Wakili: Unajua effect ya maneno yako? Unataka kufunga mwenzako miaka 20 kwanini hujaleta laptop

Shahidi: Sina nia ya kumfunga na laptop ninayo

Wakili: Wewe hujawahi kuwa mpiga picha wa Sabaya

Shahidi: Nilikuwa mpiga picha wake na hata video za YouTube kuna baadhi ya picha ninaonekana nikiwa na kamera

Wakili:Wewe unajua sauti ya Sylvester?

Shahidi:Ndiyo

Wakili:Unajua nchi hii kuna watu wana ajira wanaiga sauti za viongozi

Shahidi:Najua

Wakili:Kwanini ulienda kumuibia Mrosso

Shahidi:Sikumuibia

Wakili:Unafahamu kilicholeta matatizo yote ni Pump ambayo haikupewa risiti ya kielektroniki na usingepeleka pump watu wako wa kundi lako la mtu mwenye benzi msingemuibia Mrosso Sh90 milioni

Shahidi:Siyo kweli

Wakili:Uliwahi kuwaeleza PCCB ulikuwa na sabaya na dereva wa serikali anaitwa Kivuyo na mkaenda kwa Mrosso

Shahidi: Hapana

Wakili:Kwa hiyo umekuja kueleza baada ya Rama kukutengeneza gerezani?

Shahidi:Rama hakunitengeneza kwa chochote na hayo mambo ya kumkandamiza mtu nasikia kwako

Wakili:Unasema uliitwa Point Zone

Shahidi:Ndiyo

Wakili:Hukueleza kumuona mtu yoyote zaisi ya sabaya kati ya hawa washitakiwa wengine

Shahidi:Ni kweli nilieleza

Wakili:Hukuwaeleza kwa sababu hawakuwep

Shahidi:Sikuwaona niliona walioshuka kwenye gari

Wakili:Uliwahi kushiriki kikao chochote Point Zone

Shahidi:Sikuwahi kushiriki nimesema nilikuta magari yanatoka

Wakili:Jana ulisema mbele ya mahakama sabaya ni mtu wa hatari

Shahidi:Ni kweli

Wakili: Ulijua Sabaya ni mtu hatari lini?

Shahidi: Nilijua Sabaya ni mtu hatari 2020

Wakili: Sabaya alikupiga sana

Shahidi: Ndiyo akishirikiana na walinzi wake

Wakili: Kwa hiyo unatamani afungwe

Shahidi: Roho yangu haiko hivyo

Wakili: Unatamani aachiwe?

Shahidi:Mahakama ndiyo itaamua siwezi kuipangia

Wakili:Umesema wewe umeishi na Sabaya kama mateka?

Shahidi:Ni kweli

Wakili:Wewe unasema Sabaya amekuwa akikupiga, kukiweka lock up na matendo ya kukuumiza hivi hayo matendo ni kabla ya 20/1/2021

Shahidi:Ni kabla na baada

Wakili: Pamoja na yote hayo uliendelea bado kupokea simu zake?

Shahidi:Ndiyo maana nikasema nilikuwa mateka

Wakili: Ulisema ulilalamika kwenye vyombo vya dola lakini haikusaidia

Shahidi: Ndiyo

Wakili: Uliripoti wapi?

Shahidi:Niliripoti kwa RCO kwa bwana anaitwa Mushi na usalama wa taifa

Wakili:Wewe unashangaza sana wakati Sabaya anatoa ushahidi ulimuuliza maswali hayo na kukupiga?

Shahidi:Wakati anatoa ushahidi nilikuwa na wakili

Wakili:Kwanini hukumkataa

Shahidi:Kwa sababu sikutaka kufanya anachotaka kufanya yeye

Wakili: Kwa nini hukuwahi kuwaambia washitakiwa wenzako unawajua

Shahidi: Wakili asingetaka na kuna maswali nilikuwa nampa kwa mashahidi hapa lakini alikuwa haulizi na hata akija gerezani alikuwa anawasiliana na Sabaya. Wakili wangu mteja wake alikuwa Sabaya, hakuwa anaongea na mimi

Wakili: Kwanini hukumuuliza Enock mnafahamiana, mlikamatwa wote

Shahidi: Sikumuuliza maswali kwani sikuwa na mwelekeo wa maswali ya kuuliza

Wakili: Sasa mtu hatari kama Sabaya kwanini akutume wewe kupeleka pump?Jana ulisema alikutuma upeleke pump au kuna mzigo umpokelee?

Shahidi:Aliniambia mwenye namba hiyo anakuja na mzigo

Wakili:Je Sabaya alisema ni mzìgo gani?

Shahidi:Hakusema kabisa

Wakili:Je ni kweli kulingana na ushahidi wako aliyekuonyesha gereji ni Sabaya?

Shahidi: Aliyekuja na benzi nyeusi akitokea Bomang"ombe

Wakili:Ni kweli Sabaya hajawahi kukutumia pesa ya kulipa pump

Shahidi:Hajanitumia

Wakili:Ulienda kutengeneza pump kwa maagizo ya mwenye?

Shahidi:Kwa maelekezo ya Sabaya

Wakili:Ni kweli kwamba Sabaya aliwahi kuunda genge na wewe

Shahidi:Sijawahi kuunda genge lolote na Sabaya

Wakili:Ni kweli Sabaya, Enock waliunda genge na wewe mkaenda kwa Mrosso na kuchukua rushwa ya Milioni 90

Shahidi:Sijui mimi niliondoka pale kwa kutoroka

Wakili:Mtu anayetoroka anaweza kumfata anayemtoroka hadi Dar umbali wa kilomita 600, mtu hatari ukafika ukala chakula chake

Shahidi: Ndiyo maana niliekeza nilikuwa mateka na nilieleza sikumfata Sabaya Dar es Salaam,nilimfuata mjomba wangu

Wakili: Hivi ni kweli ulisema sabaya alikwambia maeneo hayo ni hatari

Shahidi:Niliaga naondoka akaniambia ni usiku sana siyo kuzuri kwa hiyo nipumzike nitaondoka asubuhi

Wakili:Mtu anayekutesa anaweza kuwa concerned na security yako?

Shahidi:Alifanya hivyo kwa sababu nilichukua mzigo wake na kumpelekea Dar

Chanzo: www.tanzaniaweb.live