Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali ya Tanzania yashindwa kuwasilisha jalada kortini kesi ya Lissu

99598 Lissu+pic Serikali ya Tanzania yashindwa kuwasilisha jalada kortini kesi ya Lissu

Fri, 20 Mar 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Kesi ya uchochezi inayomkabili makamu mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu na wenzake imeshindwa kuendelea kutokana na Serikali kushindwa kuwasilisha jalada mahakamani.

Kutokana na hali hiyo, hakimu Thomas Simba wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu alionya upande wa mashataka na kuutaka tarehe ijayo ukikishe unakuwa na jalada.

“Tarehe ijayo nataka upande wa mashtaka mje na jalada ili kesi hii iendelee, maana haiwezekani mnasema hamna jalada,” alisema hakimu Simba.

Washtakiwa wengine ni Simon Mkina, Jabir Idrisa na mchapishaji wa kampuni ya Jamana, Ismail Mehboob kwa wanakabiliwa na mashtaka ya uchochezi.

Kesi hiyo jana ilipangwa kwa ajili ya kusikilizwa maombi yaliyowasilishwa na wadhamini wa Lissu wakiomba mahakama hiyo kutoa hati ya kumkamata, kwa kuwa wao wameshindwa kumpata.

Wadhamini hao, Robert Katula na Ibrahim Ahmed, waliwasilisha maombi hayo Februari 20 wakitaka mahakama hiyo itoe amri ya kumkamata Lissu baada ya jitihada za kumtafuta kushindika.

Pia Soma

Advertisement
Hata hivyo, wakili wa Serikali Ester Martin aliileza mahakama hiyo jana kuwa hawana jalada na wakili Wankyo Simon anayeendesha kesi hiyo hayupo, hivyo wanaomba tarehe nyingine ya kutajwa. Baada ya kusikiliza hoja hiyo, hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi Aprili 23.

Chanzo: mwananchi.co.tz