Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali imerejesha magari 20 yaliyoibwa nchini Kenya

6f5e4170bbaa7b69d42244bac6233402.jpeg Serikali imerejesha magari 20 yaliyoibwa nchini Kenya

Tue, 14 Sep 2021 Chanzo: www.habarileo.co.tz

MKUU wa Wilaya ya Loitokitok nchini Kenya, Wesley Koech ameishukuru na kuipongeza serikali ya Tanzania kufanikisha kukamata na kurejesha magari 20 na pikipiki zilizoibwa nchini humo.

Koech amesema hayo jana mjini Loitokitok, Kenya katika kikao cha ujirani mwema kati ya wilaya hiyo na wilaya ya Rombo, Tanzania. Koech alisema serikali ya Kenya imeimarisha uhusiano wa ujirani mwema na Tanzania na wataimarisha uhusiano na wananchi wa Rombo.

Mkuu wa Wilaya ya Taveta, nchini Kenya, Joseph Maina amesema Tanzania inastahili pongezi kwa kuwasamehe na kuwachia huru maofisa polisi wa Kenya walioingia nchini wakiwa wamebeba silaha za moto. Mkuu wa Wilaya ya Rombo, Hamisi Maigwa amesema serikali ya Tanzania imejipanga kuondoa kero na vikwazo vinavyoathiri ujirani mwema kati ya Rombo na Loitokitok.

Chanzo: www.habarileo.co.tz