Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Saudi Arabia yawanyonga watu 81 kwa siku moja

Mauajiiiiii Saudi Arabia yawanyonga watu 81 kwa siku moja

Mon, 14 Mar 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Saudi Arabia imesema iliwanyonga watu 81 siku ya Jumamosi, ambapo ni idadi kubwa zaidi ya walionyongwa mwaka jana.

Kundi hilo ikiwa ni pamoja na Wayemeni saba na raia mmoja wa Syria walitiwa hatiani kwa "uhalifu mkubwa na wa kutisha", ikiwa ni pamoja na ugaidi, shirika la habari la serikali SPA lilisema.

Baadhi walishtakiwa kwa kuwa wafuasi wa kundi la Islamic State (IS), al-Qaeda au waasi wa Houthi nchini Yemen. Mwaka jana, Saudi Arabia iliwanyonga watu 69.

Mashirika ya haki yanasema kuwa wengi hawapati kesi za haki nchini Saudi Arabia, madai ambayo serikali inayakataa.

Kwa mujibu wa SPA, kundi la hivi punde lilikuwa limehukumiwa na majaji 13 na kupitia mchakato wa kimahakama wa hatua tatu.

Walishutumiwa kwa kupanga mashambulizi dhidi ya malengo muhimu ya kiuchumi, kuua au kulenga askari wa vikosi vya usalama, utekaji nyara, utesaji, ubakaji na kuingiza silaha nchini humo.

Saudi Arabia ina moja ya viwango vya juu zaidi vya wanaonyongwa duniani ya tano katika orodha ya Amnesty International, nyingine nne zikiwa ni China, Iran, Misri na Iraq.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live