liyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya na wenzake sita wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ambayo leo Mahakama hiyo inatarajiwa kutoa hukumu ya kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili.
Mbali na Sabaya watuhumiwa wengine ni Enock Mnkeni, Watson Mwahomange, John Aweyo, Sylvester Nyegu, Jackson Macha na Nathan Msuya.
Leo Jumanne Mei 31, 2022 Sabaya na wenzake wamefikishwa mahakamani hapo saa 3:09 asubuhi
Hukumu ya leo inatarajiwa kuamua hatma ya kiongozi huyo wa zamani na wenzake endapo wataachiwa huru, kwani hadi sasa mbali na kesi hii hawana kesi nyingine.
Katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 27/2021, Jamhuri ilikuwa na mashahidi 13 huku utetezi wakiwa na mashahidi nane ambapo watuhumiwa hao walikuwa wakitetewa na jopo la mawakili watano huku Mwahomange akijitetea mwenyewe.
Machi 31 mwaka huu Hakimu Patricia Kisinda, alisema atatoa hukumu hiyo leo baada ya pande zote kuwasilisha hoja zao za majumuisho.
- Dabo awavaa Mastaa Azam FC, awapa onyo hili..!
- Duke Abuya mchezaji Bora wa mwezi Singida Big Stars
- Viongozi wa jeshi Niger waukataa ujumbe wa Ecowas
- Wakili Kibatala, Shahidi wachuana taratibu za kumtambua mtuhumiwa
- BREAKING: Sabaya na wenzake waachiwa huru kesi ya uhujumu uchumi
- Read all related articles