Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sabaya kuendelea kujitetea Jumatatu

8919c438bd54732fc5c183dc23598b7c Sabaya kuendelea kujitetea Jumatatu

Sun, 15 Aug 2021 Chanzo: www.habarileo.co.tz

MSHITAKIWA wa kwanza katika kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha, Lengai Ole Sabaya (34) ataendelea kujitetea kesho (Jumatatu) katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha.

Katika kesi hiyo, Sabaya na wenzake wawili, Silvester Nyengu (26) na Daniel Mbura (38) wanadaiwa kutumia silaha na kupora mali na Sh 3, 159,000 katika duka la Shahiid Store kwenye mtaa wa Bondeni, jijini Arusha.

Washitakiwa hao walidaiwa kufanya hivyo Februari 9, mwaka huu saa 11 jioni wakati Sabaya akiwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro.

Ilidaiwa mahakamani kuwa, kabla ya kupora, washitakiwa hao waliwashambulia watu kadhaa kwa ngumi, mateke, makofi na kichwa.

Sabaya kesho (Jumatu Agosti 16,2021) atatoa ushahidi akiongozwa na mawakili wake, Dancan Oolla na Mosses Mahuna.

Chanzo: www.habarileo.co.tz