Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeshindwa kuendelea kusikiliza kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe baada ya kuelezwa kuwa mshtakiwa huyo ambaye ni kiongozi wa chama hicho amefiwa.
Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga amedai mbele ya Hakimu Mkazi mkuu, Huruma Shaidi kuwa shauri hilo lilikuja kwa ajili ya kusikilizwa.
Soma zaidi: Shahidi kesi ya Zitto aeleza alivyowapokea majeruhi wanaodaiwa kumuua polisi
Wakili wa Utetezi, Peter Kibatala amedai leo Jumatatu Oktoba 7, 2019 kuwa mteja wake amefiwa mkoani Kigoma, anaomba mahakama ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kusikiliza kesi hiyo.
Baada ya maelezo hayo Hakimu Shaidi ameahirisha shauri hilo hadi Oktoba 22 na 23, 2019 itakapokuja kwa ajili ya kuendelea na ushahidi.
Soma zaidi: Shahidi kesi ya Zitto aeleza jinsi askari polisi, wananchi walivyouawa
Pia Soma
- Ofisa manunuzi, mzabuni wakamatwa kwa agizo la Majaliwa
- Wafariki dunia baada ya kutumbukia mtoni
- Anusurika kufa baada ya kushambuliwa na tembo
Katika kesi ya msingi, Zitto anakabiliwa na mashtaka matatu ya uchochezi anayodaiwa kuyatenda Oktoba 28, 2018 katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ofisi za makao makuu ya chama hicho.
Soma zaidi: Shahidi aliye masomoni akwamisha kesi ya Zitto