Chama cha Demokrasia na Mendeleo CHADEMA, kimethibitisha kukamatwa kwa Katibu Mkuu wa BAWACHA Taifa, Catherine Ruge , Mjumbe wa Kamati Kuu, Susan Kiwanga na viongozi wengine pamoja na wanachama 11 wa chama hicho nje ya mahakam ya Hakimu Mkazi Kisuti
Wanachama hao walifika Mahakamani hapo kwaajili ya kusikiliza kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa chama hicho licha ya maarufuku iliyotolewa na Jeshi la Polisi iliyowataka kutokusanyika katika viunga vya Mahakama hiyo
Tangu kukamatwa kwa Mbowe, kumekuwa na taaarifa za kushikiliwa kwa wafuasi wa CHADEMA katika maeneo tofauti tofauti nchini ambao wamekuwa wakisisitiza kuachiwa kwa kiongozi huyu, huku wakiwa na ujumbe Mkuu unaosema "Mbowe sio Gaidi"