Jeshi la Polisi limethibitisha kutokuwepo kwa vitendo vya uhalifu katika Wilaya za Kibiti, Mkuranga na Rufiji zilizopo mkoani Pwani.
Haya yamethibitishwa na Msemaji Mkuu wa Jeshi Polisi nchini, David Misime, ambaye alieleza kuwa wamefanya operesheni maalumu kwenye wilaya hizo zilizolenga kuwabaini wahalifu na wanaofanya mauaji kwenye maeneo hayo.
"kama mtakumbuka, tulishuhudia vitendo vya uhalifu, vilivyotishia hali ya usalama, kama vile, vitendo vya ukabaji na ugaidi kwenye wilaya za kibiti na Rufiji hasa kuanzia mwaka 2014 hadi 2017. Hivyo tumeendesha operesheni hii maalum kuanzia julai 31 hadi Agosti 2 mwka huu ili kuhakikisha maeneo hayo yanakuwa salama"
Kamanda huyo alieleza kuwa zoezi hilo lilifanywa kwa kushirikiana na vyombo vingine vya Ulinzi na usalama pamoja na wakazi wa maeneno hayo, na kufanikiwa kukamata silaha pamoja na watu waliokisiwa kujihusisha na vitendo hivyo uhalifu.