Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Polisi yawakamata raia wanne wa kigeni

81589 Raia+pic Polisi yawakamata raia wanne wa kigeni

Fri, 25 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linawashilia raia wanne wa Ethiopia na Somalia kwa madai ya kuingia nchini Tanzania kinyume na sheria.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Oktoba 24, 2019 kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto amesema wahamiaji hao walikamatwa wilayani Mpwapwa wakitoka Arusha kuelekea Iringa wakiwa katika pikipiki.

Amesema polisi pia wanawashikilia Watanzania wawili waliokuwa wakiwasafirisha raia hao wa kigeni kutoka Arusha kwenda Iringa.

Amewataja watu hao kuwa ni Sellamu Yohanes na Ashetu Tefaye (Waethiopia), Mahamoudu Mapaa na Cuse Ciise (Wasomali). Amesema Watanzania waliokamatwa ni Jamali Martin na Wiston Makia.

“Pia watuhumiwa walikuwa na Sh1 milioni walizokuwa wamepanga kuwahonga askari wetu ili wasiwakamate lakini walikataa rushwa hiyo,” amesema Muroto.

 

Pia Soma

Advertisement

Chanzo: mwananchi.co.tz