Wed, 29 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Watu sita wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Singida wakihusishwa na mauaji ya watu, ufukuaji wa makaburi na kuchukua viungo, baadhi ya vitu vya maiti katika maeneo tofauti wilayani Manyoni.
Imeelezwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Stella Mutabihirwa, leo Machi 28, 2023 kuwa hatua hiyo imefuatia msako uliofanywa na Jeshi hilo, kati ya Machi 16 na 24 Mwaka huu.
“Msako ulifanyika kwenye maeneo tofauti ya Wilaya ya Manyoni na vijiji vya jirani vilivyopo Wilaya ya Sikonge mkoani Tabora,” amesema Kamanda Mutabihirwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live