Rombo. Wanafunzi wiwili wa kidato cha tatu Shule ya Sekondari Kilamfua wilayani Rombo Mkoa wa Kilimanjaro wamebakwa na mwanaume mmoja wakiwa katika hifadhi ya mlima Kilimanjaro wakiokota kuni.
Akizungumza leo Jumatano Julai 3, 2019 kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Hamis Issah amesema tukio hilo limetokea jana Julai 2, 2019.
Amesema kwa mujibu wa wanafunzi hao wenye umri wa miaka 15, wakati wakiendekea kuokota kuni alitokea mtu huyo ambaye hawakumtambua na kuanza kuwafanyia kitendo hicho cha kikatili.
Issah amesema wanafunzi hao wanaopatiwa matibabu katika Hospitali ya Huruma wamedai mtu huyo alianza kumbaka mmoja baada ya mwingine.