Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha, linamshikilia Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Mhe: Tundu Lissu pamoja na wenzake watatu wa Chama hicho kwa ajili ya mahojiano kuhusiana na tuhuma za kufanya mikusanyiko isiyo ya halali na kuwazuia Askari Polisi kutekeleza majukumu yao.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha, linamshikilia Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Mhe: Tundu Lissu pamoja na wenzake watatu wa Chama hicho kwa ajili ya mahojiano kuhusiana na tuhuma za kufanya mikusanyiko isiyo ya halali na kuwazuia Askari Polisi kutekeleza majukumu yao. Baada ya mahojiano hayo na ukamilishwaji wa taratibu zingine, hatua nyingine za kisheria zitafuata.