Tue, 5 Feb 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Tabora. Polisi mkoani Tabora wanamshikilia mkazi wa kitongoji cha Utemini kata ya Ushokola wilayani Kaliua, Amos Zakaria kwa tuhuma za kumbaka mtoto wa miaka sita.
Akizungumza leo Jumatatu Februari 4, 2019 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Emmanuel Nley amesema tukio hilo limetokea jana saa sita mchana.
Amesema mtuhumiwa alimvizia binti huyo wakati anapita na kumvutia bafuni kisha kumbaka.
Amesema polisi walimkamata na baada ya kukamilisha maelezo atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.
Chanzo: mwananchi.co.tz