Arusha. Polisi mkoani Arusha nchini Tanzania limemkamata na kumuhoji Salim Ibrahim (56) ambaye ni baba wa mwanafunzi, Faisal Salimu (19) aliyejiua kwa kujipiga risasi jana Jumapili alfajiri Agosti 18,2019.
Kamanda wa polisi mkoa Arusha, Jonathan Shana akizungumza na Mwananchi leo Jumatatu Agosti 19,2019 amesema baada ya mahojiano polisi imemwachia Ibrahim.
"Tulimchukua kwa mahojiano baba wa mtoto huyu na baada ya uchunguzi wa awali tumemwachia na uchunguzi unaendelea," amesema Shana.
Hata hivyo, amesema sheria zipo kwa watu wanaomiliki silaha kutakiwa kuhifadhi vyema silaha zao.
Mwanafunzi huyo wa kidato cha tano, Shule ya Arusha Meru alijiua kwa kujipiga risasi kwenye paji la uso akiwa chumbani kwake katika nyumba anayoishi na baba yake pekee mkoani Arusha.
Tayari mwili wa mwanafunzi huyo umezikwa jana Jumapili.