Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Polisi Tanzania wakamata vipodozi vyenye sumu

69583 Pic+polisi

Sat, 3 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Morogoro. Jeshi la polisi Mkoa wa Morogoro limekamata shehena ya vipodozi vyenye viambata vya sumu zilivyokuwa vikisafirishwa kutoka Zambia kuelekea Dar es Salaam.

Akizungumza leo Ijumaa Agosti 2, 2019 kamanda wa polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa amesema maboksi 230 ya vipodozi hivyo yamekamatwa leo eneo la Chamwino barabara ya Morogoro- Iringa.

Amesema taarifa za kusafirishwa kwa vipodozi hivyo imetolewa na raia wema waliowapa habari polisi waliokuwa doria katika barabara hiyo, kuliwekea gari hilo kizuizi ambalo pia lilikuwa limepakia mchanga wa shaba.

Kamanda Mutafungwa amemtaja dereva wa gari hilo kuwa ni Sudi Mnukwa na msindikizaji wa vipodozi hivyo Samson Emanuel wote wakazi wa jijini Dar es Salaam.

Amebainisha kuwa baada ya kuhojiwa walieleza kuwa vipodozi hivyo walivipakia Tunduma ambako ni mpakani mwa Tanzania na Zambia.

Amesema kuwa pamoja na kuwashikilia watuhumiwa hao, gari lililobeba vipodozi hivyo limezuiwa.

Pia Soma

Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Morogoro, Emmanuel Maro amesema pamoja na watuhumiwa kusafirisha vipodozi hivyo vyenye viambata vya sumu lakini pia walikuwa wakisafirisha bila ya kulipa kodi na hivyo kuipotezea mapato nchi.

Chanzo: mwananchi.co.tz