Jeshi la Polisii mkoani Shinyanga limekamata bastola yenye namba 07IT4823, ikiwa na risasi tano kwenye begi lililotelekezwa na vijana waliokuwa wamepandishana zaidi ya wawili katika pikipiki ‘bodaboda’.
Jeshi la Polisii mkoani Shinyanga limekamata bastola yenye namba 07IT4823, ikiwa na risasi tano kwenye begi lililotelekezwa na vijana waliokuwa wamepandishana zaidi ya wawili katika pikipiki ‘bodaboda’. Kamanda wa Polisi Mkoa Shinyanga, Janeth Magomi, amesema vijana hao wakiwa wamepakizana katika bodaboda eneo la Msalala, Wilaya ya Kahama, walionekana kuwa wasiwasi, hivyo kuanza kuwafuatilia na ndipo wakatelekeza pikipiki yao pamoja na begi hilo na kukimbia.