Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Papa Msofe, mwenzake waunganishwa kesi ya uhujumu uchumi

95308 Pic+musofe Papa Msofe, mwenzake waunganishwa kesi ya uhujumu uchumi

Tue, 11 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Washtakiwa wawili akiwemo mfanyabiashara Marijan Msofe maarufu Papa Msofe wameunganishwa katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili wakili wa kujitegemea, Abdul Lyama.

Msofe na Fadhili Mganga wanakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu dola 26, 250 za Kimarekani sawa na zaidi ya Sh60 milioni.

Wakili wa Serikali, Grory Mwenda akisoma hati ya mashtaka leo Jumanne Februari 11, 2020 mbele ya Hakimu Mkazi mwandamizi wa Mahakama ya Kisutu, Augustina Mmbando amedai washtakiwa kwa pamoja wanakabiliwa na shtaka la kuunda genge la uhalifu, utakatishaji fedha na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Mwenda amedai kati ya Januari Mosi, 2019 na Desemba 30, 2019 jijini Dar es Salaam washtakiwa waliunda genge la kihalifu huku akijua kufanya hivyo ni kosa la kisheria.

Katika shtaka la pili, wanadaiwa tarehe hiyohiyo jijini Dar es Salaam walijipatia dola 26, 250 za kimarekani sawa na zaidi ya Sh60 milioni wakijua fedha hizo ni zao la jinai la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Shtaka la mwisho wanadaiwa tarehe hiyo jijini Dar es Salaam washtakiwa walijipatia dola 26, 250 za kimarekani sawa na zaidi ya Sh60 milioni kutoka kwa Yasser Moawed Abdelhamad wakimdanganya kumuuzia tani 25 za madini ya Shaba huku wakijua siyo kweli.

Habari zinazohusiana na hii

Advertisement
Mwenda amedai bado upelelezi haujakamilika na kuomba mahakama kuahirisha shauri hilo

Hakimu Mmbando ameahirisha shauri hilo hadi Februari 25, 2020 itakapokuja kwa ajili ya kutajwa.

Msofe anakabiliwa na kesi nyingine pamoja na wenzake watano. Wanakabiliwa na mashtaka matano likiwamo la kujipatia Sh943 milioni kwa njia ya udanganyifu.

Chanzo: mwananchi.co.tz