Thu, 23 Nov 2023
Chanzo: Global Tv
Wananchi wa Kichangani kata ya Mwandege wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani wamejeruhiwa kwa kukatwa mapanga na kuibiwa baadhi ya vitu vyao vya ndani ikiwemo televisheni na watu wanaodhaniwa kuwa ni panya road.
Global Tv imefika mpaka eneo la tukio na kufanya mahojiano na baadhi ya majeruhi wametoa ushuhuda namna ambavyo Panya Road hao walivyowajeruhi wananchi hao na kuiba baadhi ya vitu vya ndani.
Wananchi wameiomba serikali kuingilia kati suala hilo kwani vijana hao wanaweza kusababisha maafa makubwa.
Video kamili inapatikana YouTube ya Global Tv Online
Chanzo: Global Tv