Mwenyekiti wa Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania,Chama Cha Demokrasia na Maendeleo( CHADEMA),Freeman Aikael Mbowe anatarajia kufikishwa mahakamani leo Agosti 6 kusikikiliza mashitaka yanayomkabili.
Mbowe anashitakiwa kwa makosa ya Ugaidi na kupanga njama za kuua Viongozi wa serikali na atafikishwa mahakamni Jijini Dar es Salaam na kusomewa mashitaka yake.
Wakati huo huo Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro,amewaonya wanachama wa Chama hicho akisema si ruhusa kufanya maandamano wala kukusanyika katika maeneo ya Mahakama,lakini Viongozi wa CHADEMA wamesisitiza watahudhuria kwa wingi Mahakamani hapo wakati wa kusikilizwa shauri hilo kwa kuwa Mahakama ni muhimili huru na hakuna Sheria inayowazuia watu kusikiliza kesi mahakamani.
Mbowe alikamatwa mwezi uliopita Jijini Mwanza alipokwenda Kuhudhuria Kongamano la Kushinikiza Katiba Mpya.