Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Khamis Hamza Chilo, amesema Serikali imeanzisha Operesheni Maalumu ijulikanayo kwa jina la “Operesheni Punguza Mahabusu” lengo ikiwa ni kupunguza msongamano wa mahabusu katika magereza mbalimbali nchini.
Submitted by Elbogast on Jumapili , 11th Jul , 2021 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Khamis Hamza Chilo akisalimiana na maaskari wa gereza la Ruanda.
Waziri Khamis Hamza Chilo amesema hayo wakati akizungumza katika kikao kilichohusisha wafungwa na Mahabusu wanawake katika Gereza la Ruanda jijini Mbeya.
Mbali na hilo pia aliwapa vitu mbalimbali ikiwemo magodoro, Taulo za Kike, Miswaki na sabuni.