Tue, 23 Jul 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Mwanza. Ofisa mfawidhi wa rasilimali za uvuvi kanda ya Ukerewe mkoani Mwanza ameuawa na wananchi baada ya kuibuka vurugu kati ya wakazi wa kisiwa cha Siza wilayani Ukerewe na polisi.
Katika vurugu hizo watu wengine watatu wameuawa kwa kupigwa risasi huko polisi mmoja akijeruhiwa.
Akizungumza na Mwananchi jana jioni Jumatatu Julai 22, 2019 mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella amesema vifo hivyo vimetokana n na vurugu baada ya askari polisi waliokuwa wameongozana na kikosi cha kuzuia uvuvi haramu kufika kisiwani humo.
Endelea kufuatilia Mwananchi kwa taarifa zaidi
Chanzo: mwananchi.co.tz