Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ofisa mwingine polisi aunganishwa kesi kupokea rushwa ya Sh200 milioni

80413 Pic+kesi

Thu, 17 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Ofisa mpelelezi wa kituo cha Polisi Kawe, Emmanuel Njegele ameunganishwa na wenzake watatu katika kesi ya kuomba na kupokea rushwa ya Sh200 milioni.

Mbali na Njegele, maofisa wengine wa watatu wa kituo hicho, Shaban Shillah, Joyce Kita na Ulimwengu Rashid walifikishwa mahakamani hapo Oktoba 3, 2019.

Njegele ameunganishwa leo  na wenzake baada ya mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutoa hati ya kukamatwa ambapo amesomewa mashtaka tisa mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustine Rwizile

Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Nickson Shao amemsomea mshtakiwa huyo makosa yanayomkabili ambayo aliyakana na kuelezwa kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Mshtakiwa huyo alitimiza masharti na kuachiwa kwa dhamana na kesi hiyo kuahirishwa hadi Novemba 15, 2019 itakapotajwa tena.

SOMA ZAIDI: Vigogo polisi kizimbani kwa madai ya kuomba rushwa ya Sh200 milioni

Pia Soma

Advertisement

Chanzo: mwananchi.co.tz