Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ofisa madini Manyara kizimbani kwa rushwa

98215 Pic+madini Ofisa madini Manyara kizimbani kwa rushwa

Fri, 6 Mar 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Babati. Ofisa wa madini mkazi mkoa wa kimadini Simanjiro, Daudi Ntalima amefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Manyara kwa tuhuma ya kuomba rushwa ya Sh5 milioni kwa wakurugenzi wa kampuni ya Tanzanite One.

Mwendesha mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Eveline Onditi akisoma hati ya mashtaka leo Ijumaa Machi 6, 2020 amedai mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Februari 21, 2020.

Mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa huo,  Simon Obero mwendesha mashtaka huyo amedai mshtakiwa huyo alitenda makosa hayo huku akijua ni kinyume cha sheria.

Amedai kuwa mshtakiwa aliomba rushwa hiyo kwa wakurugenzi wa kampuni hiyo, Hussein Gonga na Faisal Shabahi.

Amedai alitenda kosa hilo kwenye eneo la mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro kinyume na kifungu cha 15 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007.

Hata hivyo, hakimu Obero alipomuuliza mshtakiwa huyo kama ni kweli alitenda kosa hilo alikana mashtaka hayo.

Pia Soma

Advertisement

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Aprili 21, 2020 itakapotajwa tena mahakamani hapo. Mshtakiwa huyo yupo nje kwa dhamana.

Chanzo: mwananchi.co.tz