Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nyalandu aripoti polisi, ahojiwa Takukuru

60327 Pic+nyalandu

Thu, 30 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Singida. Aliyekuwa mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu na wenzake watatu leo Jumatano Mei 29, 2019 wameripoti kituo cha polisi kati mkoani Singida na kutakiwa kwenda tena kituoni hapo Mei 31, 2019 kwa ajili ya mahojiano.

Nusu saa tangu wafike kituoni hapo, walichukuliwa na maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupabana na Rushwa (Takukuru)  na kuhojiwa kuanzia saa 3 hadi saa 4 asubuhi, kisha  kuachiwa kwa dhamana ya Sh5milioni kila mmoja.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Nyalandu amesema baada ya kuhojiwa wametakiwa kuripoti polisi Ijumaa huku Takukuru wakiwataka kuripoti Juni 19, 2019.

Amesema wakiwa polisi hawakuhojiwa zaidi ya kutakiwa kurejea tena Ijumaa

“Inashangaza  lakini ninawaomba makamanda wote (wanachama wa Chadema) kuwa na utulivu wasilipe ubaya kwa ubaya ila walipe ubaya kwa wema, “amesema Nyalandu.

Nyalandu alikamatwa na Takukuru Jumatatu Mei 27, 2019 katika kata ya Itaja jimbo la Singida Kaskazini, akituhumiwa kwa makosa mawili ya rushwa na kuendesha mkutano bila kibali.

Habari zinazohusiana na hii

Hata hivyo,  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Sweetbert Njewike jana aliwaeleza waandishi wa habari kuwa jeshi hilo halina shida yoyote na watuhumiwa hao ila Takukuru waliomba polisi kuwahifadhi.

Chanzo: mwananchi.co.tz