Serengeti. Polisi wilayani hapa mkoa wa Mara wamemkamata mtuhumiwa mmoja kati ya wawili wanaodaiwa kumbaka mama mmoja mwenye umri wa miaka 58, mkazi wa Miseke
ambaye amelazwa hospitali Teule ya Nyerere kwa ajili ya matibabu.
Tukio hilo linadaiwa kutokea Aprili 6 usiku katika kitongoji cha Senta wakati mama huyo (jina limehifadhiwa), mkazi wa kitongoji cha Majengo akitoka kutafuta tumbaku na mboga na inadaiwa watuhumiwa walimfuatilia kwa nyuma na kumkaba na kumfanyia ukatili huo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara, Daniel Shillah aliliambia Mwananchi kwa njia ya simu jana kuwa mtuhumiwa Kumari Mongita (23) mkazi wa kijiji cha Miseke amekamatwa na mmoja wanaendelea kumtafuta kwa kuwa alikimbia.
“Watuhumiwa walitajwa na mama huyo aliyefanyiwa ukatili na vijana hao, huyo mmoja kwa ushirikiano na wananchi tunaamini atakamatwa ili wafikishwe mahakamani baada ya taratibu kukamilika,” alisema .
Mganga mkuu wa hospitali ya Nyerere, Tanu Warioba alidai mama huyo ana maumivu kifuani na sehemu nyingine za mwili.
Pia Soma
- Ujumbe wa Butiku kuhusu corona
- Mwili wa askari wakutwa mtaroni karibu na kituo cha polisi
- SIMULIZI: Sauti ya marehemu yasikika kwa binti ataja waliomuua-VIDEO