Nairobi, Kenya. Unaweza kufikiria ni tamthilia lakini ni kweli imetokea nchini Kenya baada ya mtu anayesadikiwa kuwa mwizi kuvunja madhabau ya kanisa kwa lengo la kuiba kuacha barua ya kuomba radhi.
Mtu huyo alifanya tukio hilo usiku wa kuamkia Jumapili katika Kanisa la Pentekosti Nyandarua lililopo jijini Nairobi Kenya.
Inadaiwa kuwa mwizi huyo aliandika ujumbe huo bada ya kukosa fedha katika madhabau hayo.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation la Kenya, tukio hilo litokea miezi michache baada ya uongozi kukamata watu watatu wanaosadikiwa kuhusika na wizi katika kanisa hilo.
Barua hiyo iliyosomwa kwa waumini wakati wa ibada ya Jumapili, mwizi huyo alisema anajutia kitendo alichofanya na kuomba asamehewe.
“Nimeelekezwa na mmoja wa waumini ambaye aliniambia fedha zinahifadhiwa ndani ya kanisa, lakini nilipofika sikukuta kiasi chochote, Mungu awabariki na mniombee,” ilisema sehemu ya barua hiyo.
Pia Soma
- Polisi waendelea kumng’ang’ania Halima Mdee
- VIDEO: Magufuli azindua nyumba za askari, atoa agizo kwa IGP Sirro
- Polisi yatimua askari wake 54, Magufuli apigilia msumari
“Tulikuta barua ndani ya kanisa wakati polisi walipofika kwa ajili ya upelelezi wa tukio hilo. Aliamini kuna kiasi kikubwa cha fedha ndan; tumemsamehe na tunamuombea aokoke. Tunamkaribisha aje kutubu na kusali pamoja nasi,” alisisitiza Mchunaji Wanyoike.