Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanyika wa Acacia na wenzake watimiza siku 498, gerezani bila upelelezi kukamilika

97450 Pic+mwanyika Mwanyika wa Acacia na wenzake watimiza siku 498, gerezani bila upelelezi kukamilika

Sat, 29 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Aliyekuwa raisi wa Migodi ya Pangea, North Mara, Exploration na Bulyanhulu, Deogratius Mwanyika(56) na wenzake, wametimiza siku 498 wakiwa rumande, huku upelelezi wa kesi hiyo ukiwa bado haujakamilika.

Washtakiwa hao walifikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Oktoba 17, 2018 wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 77/2018.

Kesi ya vigogo wa Acacia mambo ni yale yale

Mwanyika wa Acacia, mwenzake washtakiwa kwa makosa 39

Mwanyika na wenzake sita, wanakabiliwa na mashtaka 39, yakiwemo ya utakatishaji fedha na kukwepa kodi.

Leo, Ijumaa Februari 28, 2020 Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon ameieleza mahakama hiyo, mbele ya Hakimu Mkazi, Vick Mwaikambo kuwa kesi hiyo iliitwa Mahakama hapo kwa ajili ya kutajwa.

Pia Soma

Advertisement
"Kesi ilikuja kwa ajili ya kutajwa na hakimu anayesikiliza shauri hili( Godfrey Isaya) ana udhuru, hivyo tunaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa," amesema wakili Simon.

Baada ya kueleza hayo, hakimu Mwaikambo aliahirisha kesi hiyo hadi Machi 13, 2020 itakapotajwa.

Washtakiwa wamerudishwa rumande kutokana na mashtaka ya kutakatisha fedha yanayowakabili kutokuwa na dhamana kwa mujibu wa sheria.

Mwanyika atakiwa kwenda kwa DPP

Upande wa mashtaka kesi ya Mwanyika waomba msaada wa upelelezi nje ya nchi

Mahakama yakataa kubadili jina la Mwanyika

Upelelezi vigogo Acacia wasubiriwa kutoka nje

Mwanyika wa Acacia, wenzake waendelea kusota rumande

Chanzo: mwananchi.co.tz