Katika hali isiyo ya kawaida mwanaume mmoja ajulikanae kwa jina la Kichele Marwa mwenye umri wa miaka 48 mkazi wa mtaa wa Igelegele kata ya Mahina mkoani Mwanza anadaiwa kuwawekea sumu kwenye uji watoto wake wa kambo kwa lengo la kuwauwa ili aishi vizuri na mama yao
Mama mzazi wa Watoto hao Deniza Felician amesema Mume wake huyo amekua akigombana nae mara kwa mara kuhusu Watoto hao watatu aliomkuta nao akitaka awaondoe nyumbani hapo hadi ilipofika siku ya tukio hilo alipoamua kuweka sumu kwenye uji ili awauwe.
Baadhi ya majira wa mama huyo wamesema wamekua wakishuhudia matukio ya ugomvi ya mara kwa mara katika famili hiyo.
Balozi wa mtaa huo ambae amekua akipokea taarifa za malalamiko kutoka kwa mama huyo amesema tayari hatua za kisheria zimechukuliwa dhidi ya Kichele Marwa.