Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanafunzi amuua kwa kumchoma kisu mjamzito, awanyonga wanaye wawili

Kifo Mauaji Wachimbaji Madini?fit=640%2C426&ssl=1 Mwanafunzi amuua kwa kumchoma kisu mjamzito, awanyonga wanaye wawili

Wed, 6 Jul 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Huzuni umeghubika katika Kijiji cha Poroko katika kaunti ndogo ya Trans Mara Magharibi nchini Kenya baada ya kijana mwanafunzi wa darasa la nane kumuua kinyama mwanamke mjamzito na watoto wake wawili.

Jeshi la Polisi nchini humo limesema linamshikilia mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 17, ambaye anadaiwa alimuua mwanamke huyo kwa kumdunga kisu kichwani, kifuani na sehemu nyingine za mwili, kisha kuwaua watoto wake wawili kwa kugeuza shingo zao kabla ya kutupa miili yao katika shamba la mahindi lililo mbali na nyumbani kwao.

Imeelezwa kuwa, jamaa na majirani wa mshukiwa wamesema kuwa wanahisi huenda kulikuwa na ugomvi kati ya mshukiwa na marehemu kabla ya kuzua mashambulizi.

Polisi wamethibitisha kuwa, kijana huyo alikuwa akitumikia kifungo cha nje kwa kuiba redio, vikombe na sahani kutoka kwa marehemu anayesemekana kuwa ndugu yake wake.

Kwa kuwa kumfunga nduguye kunaweza kuhatarisha uhusiano wake na jamaa wa karibu, mwanamke aliyeuawa aliwasihi polisi wasimfunge mshukiwa.

“Naelewa kijana huyo anatoka kwa jirani tu, naambiwa alishukiwa kumuibia marehemu wakati fulani. Inashangaza kwamba nyumba hii italazimika kuzika watu wanne kwa sababu hospitali imethibitisha kuwa wataondoa mtoto ambaye hajazaliwa na kuzikwa kando. Hiki ni kitendo cha uhalifu na hatuwezi kukielezea kwa maneno mengine," Dominic Olonana, mkazi wa eneo hilo," alisema.

Majirani na jamaa waliobaini kuwa mvulana huyo alikuwa mhalifu mashuhuri pia waliambia polisi kuwa visa vya uhalifu vilikumba eneo hilo hivi majuzi. Kwa sasa wamewataka polisi kuzidisha msako wa kuwasaka wahalifu ili kurejesha hali ya usalama na utulivu katika kijiji hicho.

“Polisi waimarishe doria na kuwatoa wahalifu hawa ili kufanya eneo hilo kuwa salama. Watu hawawezi kuzingirwa na wahalifu hawa kiasi kwamba raia wapenda amani wanaogopa kutoka nje ya nyumba zao usiku. Je, wanataka wanakijiji wahamie mjini ambako kuna polisi." Samson Leteipa, ndugu wa karibu wa mtuhumiwa alilalamika.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live