Mwanafunzi wa shule ya Msingi Olengashu wilayani Kiteto mkoani Manyara, Mesia Samwel Munga (14) amepoteza maisha kwa kujinyonga na kamba ndani ya nyumba yao asubuhi ya leo Februari 29, 2024, baada ya wazazi wake kwenda shamba.
Mwanafunzi wa shule ya Msingi Olengashu wilayani Kiteto mkoani Manyara, Mesia Samwel Munga (14) amepoteza maisha kwa kujinyonga na kamba ndani ya nyumba yao asubuhi ya leo Februari 29, 2024, baada ya wazazi wake kwenda shamba. Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara SACP George Katabazi amethibitisha tukio hilo na kusema wanaendelea na uchunguzi ili kubaini sababu iliyopelekea kuchukua hatua za kujitoa uhai.